BREAKING NEWS

Comments

Saturday, November 11, 2017

MAJANGA TENA MAN UNITED, PHILI JONES AUMIA AKIICHEZEA ENGLAND


Beki wa kati Phil Jones alilazimika kutomaliza mchezo wa timu yake ya taifa ya England baada ya kuumia wakati ilipokuwa ikikipiga dhidi ya Ujerumani, jana katika mchezo wa kirafiki.
Kuumia kwa beki huyo kunaweza kuongeza pigo kwa Manchester United chini ya Kocha Jose Mourinho.
Mourinho amekuwa na wachezaji kadhaa majeruhi akiwemo straika mkongwe Zlatan Ibrahimovic ambaye yupo njiani kurejea uwanjani kutoka katika majeraha ya goti.
Phil Jones aliumia katika mchezo huo uliofanyika kwenye Uwanja wa Wembley ikiwa ni mchezo wa kirafiki.
Jones alianza kuchechemea kuanzia katika dakika ya 10 lakini baadaye aliendelea hadi dakika ya 24 alipotoka. 

Share this:

Post a Comment

 
Back To Top
Copyright © 2014 JAMII FOCUS. Designed by OddThemes